TUTUNZE MAZINGIRA YATUTUNZE ASEMA PHILEMONI KIEMI MKOANI SINGIDA

Mkurugenzi   Wa Kijiji cha Nyuki Bw. Philemon Kiemi pamoja na Mjumbe Wa  Mkutano Mkuu CCM Bw. Ahmed Misanga Leo Wamezindua Upandaji miti elf 5000 Pembezoni  Mwa  Barabara ya Kisaki - Wilayani  Ikungi Mkoani Singida  na ndani ya shamba la ufugaji nyuki Linalo Milikiwa na Kampuni ya Kijiji cha nyuki.

 Mkurugenzi wa Kijiji Cha Nyuki Bw Kiemi Amesema  Kijiji cha nyuki tumeamua kuwekeza katika upandaji miti kwa kuzingatia kwamba Nyuki wana mchango Mkubwa katika maisha ya binadamu na mazingira kwa ujumla na hasa umaarufu wake wa kuzalisha chakula  Kisichooza ambacho ni Asali na mazao yake mengine...


 Bw Kiemi Ameendelea kusema kuwa Manufaa ya nyuki yanaenda mbali zaidi ya Asali hadi kwenye uzalishaji wa vyakula mbalimbali vya kawadia , Dawa na pia utunzaji wa mazingira kwani nyuki ni sehemu muhimu ya ukuaji uendelevu wa mimea kutokana na Uchavushaji (Pollination).

 Aidha Bw. Kiemi Amesema Kuwa Kwa sasa wadudu hao wako hatarini kutokana na uchafuzi na uharibifu wa misitu na mazingira kwa kuzingatia Hilo kampuni ya Kijiji cha Nyuki Tumeamua kuwekeza katika upandaji miti elf 10 kila mwaka na kuhaikisha miti Hiyo Inakuwa.

Kwa Upande Wa Mjumbe Wa Mkutano Mkuu Wa CCM Bw. Ahmed Misanga  Amesema Tunza Mazingira Yakutunze,Na Amewaomba Wananchi Na Viongozi Mbali Mbali Kupanda miti Katika Maeneo Yao Na kuhamasisha Wadau Kuendelea Kupanda Miti  Kwajili Ya Masilahi Ya Taifa Na Jamii Kwa Ujumla.

                          
                           
   Na Mwandishi Wetu Singida.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments