UTEUZI: RAIS SAMIA AFANYA MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI, MAKATIBU WAKUU

Rais Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mawaziri, ambapo amemhamisha Mohamed Mchengerwa aliyekuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo kwenda kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.

Kupitia taarifa iliyotolewa leo Jumanne Februari 14, 2023 na Mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais ikulu Zuhura Yunus imeeleza kuwa Kabla ya mabadiliko hayo nafasi hiyo ya Waziri wa Maliasili na Utalii illikuwa ikishikiliwa na Dkt. Pindi Chana.Dkt. Pindi Chana amehamishiwa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Pia Dkt. Samia amefanya mabadiliko madogo kwa Makatibu Wakuu wa wizara ambapo Dkt. Hassan Abbasi amehamishwa na kuwa Katibu Mkuu wa wizara ya Maliasili na Utalii akitokea wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Nafasi hiyo ilikuwa ikishikiliwa na Profesa Eliamani Sedoyeka.

Said Othman Yakub ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Dkt. Abbasi.

Kabla ya uteuzi huo Yakub alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Viongozi hao wataapishwa hapo kesho saa 10 jioni Ikulu, Dar es Salaam.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments