Daraja la kuunganisha Zanzibar, Tanzanzia Bara mbioni kujengwa

Serikali imeanza mazungumzo kuhusu ujenzi wa daraja litakalounganisha Tanzania Bara na Zanzibar ili kurahisisha usafiri kwa pande zote mbili.

Kauli hiyo imetolewa bungeni leo Ijumaa Aprili 28, 2023 na Naibu Waziri wa Ujenzi na uchukuzi, Geofrey Kasekenya ambaye amesema mazungumzo hayo yalifanyika Machi 11, 2023.

Naibu Waziri alikuwa akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum Mwantumu (CCM), Dau Haji ambaye ameuliza Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja linalounganisha Tanzania Bara na Zanzibar.



TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments