Dereva ajali iliyoua 13 Songea anaswa akitoroka

Takribani wiki moja tangu kutokea kwa ajali iliyoua wafanyabiashara 13 na kujeruhi wengine 12 katika Kijiji cha Namatui wilayani Songea, Mkoa wa Ruvuma, Jeshi la Polisi limemkamata Dereva Thobias Njovu (47), akidaiwa kuwa kwenye harakati za kutoroka.

Ajali hiyo ilitokea usiku wa Aprili 9 mwaka huu ambapo, Njovu, mkazi wa Lizabon Manispaa ya Songea akiendesha gari hilo aina ya ya Mitsubishi Fuso lilitumbukia mtoni.

Mara baada ya ajali hiyo, Njovu alitoweka kusikojulikana na jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Marco Chilya aliliambia gazeti hili kuwa wamemkamata.


“Leo (jana) saa nne asubuhi katika stendi ya Super Feo iliyopo Mahenge tumemkamata akijiandaa kutoroka na kwa kuwa tulishasema jeshi la polisi lina mkono mrefu ndivyo ilivyotokea,” alisema.

Alisema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani Jumatatu kwa hatua zaidi za kisheria.

Kamanda huyo aliwataka wananchi kufuata sheria za usalama barabarani na madereva kuzingatia sheria kuepusha ajali zinazoweza kuepukika, ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa za waharifu ili mkoa uendelee kuwa salama.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments