Taarifa hiyo imethibitishwa na Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Pius Lutumo amesema ajali hiyo baada ya gari aina ya Toyota Hilux alilokuwa akisafiria likiendeshwa na Alex Festo kuligonga kwa nyuma gari aina ya Howo lililokuwa linaendeshwa na Rashid Mohamed.
"Tunaendelea kuwashikilia madereva wote waliokuwa wanaendesha magari hayo na chanzo cha ajali bado tunaendelea kukichunguza,"amesema
Amesema kuwa mwili wa marehemu huyo umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Pwani, Tumbi kusubiri taratibu nyingine.
Kamanda Lutumo amesema katika ajali hiyo hakuna majeruhi yoyote zaidi ya kifo cha mkurugenzi huyo na amewataka madereva kuongeza umakini pindi wawapo barabarani Ili kuepusha ajali zinazoepukika ambazo husababisha vifo, uharibifu wa mali na miundombinu.
0 Comments