SIMBA SC YAITUNGUA WYDAD 1-0, BALEKE ATUPIA

 KLABU ya Simba imefanikiwa kuondoka na ushindi wa bao 1-0 mbele ya Wydad Cassablanca katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika


Mchezo huo ambao ulipigwa kwenye dimba la Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam tumeshuhudia kandanda safi kutoka kwa wenyeji Simba sc ambao walitawala mchezo na kufanikiwa kupata bao la kuongoza kupitia kwa mshambuliaji wao raia wa DR Congo Jean Baleke akipokea pasi kutoka kwa Kibu Dennis kipindi cha kwanza.

Mpaka mapumziko Simba Sc ilikuwa mbele kwa bao moja ambalo walililinda mpaka dakika 90 na mpira kumalizika waki mbele kwa 1-0 hivyo kusubiri mechi ya marudiano ambayo itapigwa kwenye mji wa Wydad juma lijalo nchini Morocco.

Simba Sc ilianza na wacheza ambao walianza katika mechi ya wikiendi iliyopita dhidi ya watani wao wa jadi Yanga na kufanikiwa kupata ushindi.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments