Katibu mkuu wa chama cha Mapinduzi Daniel Chongolo amesema Serikali ya awamu ya sita imekuwa sikivu kwa kutatua changamoto za wananchi wakati wote
Chongolo
amesema hayo leo Mei 27,2023 muda mfupi baada ya kushiriki ujenzi
katika shule ya msingi Muungano iliyopo kata ya Boma mafinga katika
wilaya ya Mafinga ,ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku 7 ya kukagua
uhai wa chama na utekelezaji wa Ilani ya ccm 2020-2023.
Amesema
shilingi Milioni 347.5 zilizopelekwa katika shule ya Muungano kujenga
madarasa ni ushahidi tosha kuonesha namna Serikali ya CCM inavyojali
wananchi wake.
Chongolo
amewataka wakazi wa eneo hilo kutosikiliza maneno ya wanasiasa waongo
ambao wamekuwa wakiwagombanisha na Serikali yao ambayo imekua
ikitekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo
Amewataka
wazazi kuwasimamia watoto katika suala zima la elimu kwa kuwa Serikali
imeendelea kuweka mazingira mazuri ya elimu kwa watoto ikiwa ni pamoja
na kuondoa ada kwa wanafunzi kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha
sita
Awali
mkuu wa mkoa wa Iringa Halima Dendegu amesema ujenzi wa shule hiyo ya
Muungano inatokana na shule ya awali kujaa wanafunzi na hivyo Serikali
ikaona ni vema kuanzisha ujenzi mpya wa madarasa katika shule ya
Muungano.
0 Comments