Tanzania Kuunganishwa Na Masoko Ya Uhakika Ya Zao La Nyuki Ikiwemo Africa Kusini.

Rais wa Wadau wa Nyuki Nchini Apr. Philemon Kiemi ambaye ni Mwanzilishi, Mmiliki na Mkurugenzi wa Kampuni ya Kijiji Cha Nyuki Nchini Tanzania yupo kwenye Ziara ya Kikazi Nchini Africa kusini. 

Bw. Kiemi Katika Ziara hiyo,  amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi Gaudence S. Milanzi , Counselor Happiness G, na CPA Melchior N. Rweyemamu kuhusu  Kufungua Ofisi na Viwanda vya  Kijiji Cha nyuki co.ltd katika Miji ya Pretoria, Johannesburg na Capetown.

Aidha Bw. Kiemi Ameeleza kuwa hatua  ya Kampuni ya Kijiji Cha Nyuki itawasaidia Wafugaji wadogo Nchini Tanzania,  kuunganishwa na Masoko ya Uhakika ikiwepo Africa Kusini hasa  wale ambao Kwa Sasa  wako viwanja vya Bombardia Mkoani Singida wakiendelea kutafuta Masoko ya Bidhaa zao la Nyuki Kwa kushirikiana na Wadau wengine wa miradi ya Maendeleo Nchini.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments