Ubalozi wa Marekani kuadhimisha siku ya Kiswahili Duniani Dar

Mgeni maalumu katika maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (Bakita), Consolata Mushi.

Taarifa iliyotolewa na ubalozi huo, maadhimisho hayo yatayayofanyika kwenye ofisi za ubalozi yanatarajiwa kufanyika kuanzia saa 9 alasiri hadi saa 10:30 jioni.


Washiriki wa mdahalo huo watakuwa ni Kituo cha Mafunzo cha MS TCDC Arusha, wafanyakazi, wanafunzi wa Kiswahili wa Ubalozi wa Marekani, Shirika la Wamarekani wa Kujitolea (Peace Corps).

Pia, maadhimisho hayo yatawashirikisha wanaharakati wa lugha ya Kiswahili, Joram Nkumbi, Abdul Fumau ambaye ni mshairi chipukizi pamoja na Seko Shamte anayejishughulisha na kutayarisha filamu.

Mada itakayojadiliwa katika kongamano hilo ni ‘Kiswahili kinavyoimarisha Uhusiano wa Kiuchumi na Kiutamaduni kati ya Tanzania na Marekani.

Hatua hiyo ni mwendelezo wa maadhimisho ya Kiswahili duniani ambayo kilele chake kitafanyika Zanzibar, Julai 7, 2023.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments