Ilemela, Pasiansi, Buswelu zashinda Angeline Cup

TIMU za kata ya Ilemela, Pasiansi, Buswelu zimepata ushindi katika michezo yao iliyochezwa jana ya mashindano ya Angeline Jimbo cup yanayoendela Wilaya ya Ilemela Mwanza.

Ilemela imeshinda mabao 2-1 dhidi ya Buzuruga mchezo uliochezwa uwanja wa Sabasaba.

Pasiansi imeshinda mabao 3-1 dhidi ya Ibungiro katika mchezo uliochezwa uwanja wa Baptist.

Kata ya Buswelu imeshinda mabao 4-1 dhidi ya Nyamhongolo mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Buswelu Sekondari.

Timu ya Kayenze imetoka sare ya bao 1-1 dhidi ya Bugogwa katika uwanja wa shule ya msingi Bugogwa. Bao la Bugogwa lilifungwa na Elias Manyama dakika ya 5 na Sila Mipawa akaisawazishia Kayenze katika dakika ya 75.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments