Samia: Ongezeni kasi zao la mwani

 

RAIS Samia Suluhu Hassan amewataka wakulima wa zao la mwani na wanaofanya shughuli za uvuvi katika Wilaya ya Kilwa, mkoani Lindi kuzalisha kwa tija ili kujiongezea kipato.

Rais Samia amesema hayo leo Septemba 19, 2023 alipokabidhi boti 34 kwa wavuvi na wakulima wa mwani zilizotolewa kwa   mkopo wa masharti nafuu.

Amefafanua kuwa boti hizo zipo 160 zimegharimu Sh bilioni 11.5. Amewataka wavuvi hao kutunza vifaa hivyo .

Amesema boti hizo zitawarahisishia kazi zao wakati wa kupanda, kuvuna na kubebea mizigo hadi nchi kavu.

Aidha amewataka wavuvi wazalishe samaria kwa wingi kwa kuwa kuna soko la uhakika.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments