Simba inahitaji ushindi, sare tasa kufuzu makundi

  1. USHINDI au sare ya bila kufungana, itawapeleka Simba SC katika hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya mchezo wa leo kuisha sare ya mabao 2-2 dhidi ya Power Dynamos nchini Zambia.

    Simba itarudiana na timu hiyo Septemba 30, Dar es Salaam.

    Katika mchezo huo, wenyeji Dynamos walianza kutangulia kwa bao lililofungwa na Joshua Mutale dakika ya 29, bao hilo lilidumu hadi mapumziko.

    Dakika ya 60 Clatous Chama alisawazisha bao hilo na kuwa 1-1, kabla ya dakika ya 75 Cephas Mulombwa kuifungia Dynamos bao la pili.

    Dakika za mwisho Chama alifunga tena na ubao kusomeka 2-2.

    Wakati huohuo Yanga imepata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya El-Merreikh ikiwa ugenini.

    Mabao ya Yanga yalifungwa na Kenneth Musonda dakika ya 63 na Clement Mzize dakika ya 80.

    Sare yoyote itawavusha Yanga kwenda hatua ya makundi.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments