Takukuru: Mtaa kwa mtaa yawafikia maelfu

 

KAMPENI  ya mtaa kwa mtaa ya uelimishaji jamii kutambua madhara ya vitendo vya rushwa imewafikia watu  12,671  mkoani Kigoma ambapo wamepatiwa elimu ya kujua madhara ya vitendo vya rushwa sambamba na wananchi hao kutoa taarifa kuhusu tuhuma za uwepo wa vitendo vya rushwa kwenye maeneo yao.

Mkuu wa dawati la elimu kwa Umma Takukuru Mkoa Kigoma,  Leonida Mushema amesema hayo wakati akitoa taarifa yake ya utendaji kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia mwezi Aprili hadi Julai mwaka huu.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kwa niaba ya kamanda wa Takukuru mkoa wa Kigoma,Stephen Mafipa  alisema kuwa katika kipindi cha miezi hiyo mitatu maafisa wa Takukuru mkoa Kigoma walitembelea kata 14 za wilaya sita za mkoa wa Kigoma na kufanya vikao na wananchi ambapo jumla ya kero 208 ziliibuliwa.

Afisa huyo wa dawati la elimu kwa umma alisema kuwa katika kero hizo zilizoibuliwa  kero 137 zimetatuliwa huku kero 71 zikiendelea kufanyiwa kazi ambapo alibainisha kuwa Taasisi hiyo ilipokea pia  malalamiko 65 kati yake 28 yanayohusu tuhums za rushwa  na 37 yasiyohusu tuhums za rushwa na kwamba malalamiko hayo yalifanyiwa kazi na ushauri kutolewa kwa walioleta malalamiko hayo.

Katika hatua nyingine Mushema alisema kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) mkoa wa Kigoma inachunguza miradi miwili ya maendeleo kati ya miradi sita waliyokuwa wakiifuatilia yenye thamani ya shilingi bilioni 1.7.

Mkuu huyo wa dawati la elimu kwa Ummanalisema kuwa  miradi hiyo miwili inayochunguzwa ina thamani ya zaidi ya sh.milioni 43 na kwamba hatua hiyo imechukuliwa baada ya kuonekana  kuna mapungufu katika miradi hiyo ambapo mradi mmoja kati ya miradi hiyo sita walitoa ushauri kwa wahusika na marekebisho yamefanyika.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments