Kajula: AFL imeleta fursa Tanzania


DSM: OFISA Mtendaji Mkuu wa klabu ya Simba, Imani Kajula  amesema uwepo wa michuano ya African football League (AFL) una manufaa makubwa kwa taifa kutokana  na fursa mbalimbali zitazopatikana kupitia michuano hiyo.

Kajula amesema Tanzania inapaswa kujivunia kuwa  mwenyeji wa uzinduzi wa AFL.

“Licha ya kwamba ni tukio la siku moja, ila lina faida kubwa sana, kuna watu watatoka maeneo mbalimbali, kuna watakaotoka mikoani kwahiyo hiyo itakuwa pia fursa kwa wanaotaka kusafirisha mashabiki kuja Dar es salaam”amesema Kajula

Ameyasema hayo leo Oktoba 11, 2023 Dar es salaam alipokuwa akizungumzia maandalizi ya Simba kuelekea katika uzinduzi wa michuano hiyo mipya ya soka Afrika ambayo itazinduliwa  Oktoba 20, 2023 Simba ikivaana na Mabingwa wa Afrika Al Ahly ya Misri.

 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments