MKATABA WA BANDARI WASAINIWA TANZANIA

  Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya usimamizi wa Bandari (TPA) Plasduce Mbossa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TPA Mhe. Balozi Ernest Mangu wakitia saini Mkataba wa upangishaji wa Gati namba 4 mpaka 7 za Bandari ya Dar es Salaam pamoja baina ya Kampuni ya DP World ya Dubai iliyowakilishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Sultan Ahmed bin Sulayem kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 22 Oktoba, 2023.

 Waziri wa Uchukuzi Mhe. Makame Mbarawa akiwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Godius Kahyarara wakitia saini Mkataba wa Nchi Mwenyeji baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kampuni ya DP World ya Dubai iliyowakilishwa na Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Sultan Ahmed bin Sulayem kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 22 Oktoba, 2023.
Waziri wa Uchukuzi Mhe. Makame Mbarawa akipongezana na Mwenyekiti na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Sultan Ahmed bin Sulayem mara baada ya kusaini Mkataba wa Nchi Mwenyeji baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Kampuni ya DP World ya Dubai kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 22 Oktoba, 2023.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya usimamizi wa Bandari (TPA) Plasduce Mbossa pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TPA Mhe. Balozi Ernest Mangu wakitia saini Mkataba wa Uendeshaji wa Gati namba 4 mpaka 7 za Bandari ya Dar es Salaam kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 22 Oktoba, 2023.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TPA Mhe. Balozi Ernest Mangu akipongezana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya DP World ya Dubai Sultan Ahmed bin Sulayem mara baada ya kusaini Mkataba wa Uendeshaji wa Gati namba 4 mpaka 7 za Bandari ya Dar es Salaam kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 22 Oktoba, 2023.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya usimamizi wa Bandari (TPA) Plasduce Mbossa pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TPA Mhe. Balozi Ernest Mangu wakitia saini Mkataba wa Uendeshaji wa Gati namba 4 mpaka 7 za Bandari ya Dar es Salaam kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 22 Oktoba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na viongozi pamoja na wageni mbalimbali kwenye hafla ya Utiaji saini Uwekezaji na Uendeshaji wa Sehemu ya Bandari ya Dar es Salaam iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 22 Oktoba, 2023.      

Viongozi mbalimbali pamoja na wageni waliohudhuria hafla ya Utiaji saini Uwekezaji na Uendeshaji wa Sehemu ya Bandari ya Dar es Salaam iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 22 Oktoba, 2023.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments