TP, Espérance hakuna kiingilio

 


KUELEKEA mchezo wa kesho TP Mazembe wakicheza mchezo wake wa kwanza wa African Football League (AFL) katika dimba la Benjamin Mkapa dhidi ya Esperance De Tunis, mchezo huo hautakuwa na kiingilio.

TP Mazembe wamechagua kutumia uwanja wa Benjamin Mkapa na inakuwa faida kwa Tanzania kushuhudia michezo mingine zaidi ya Africain Football League ambayo inasimamiwa na FIFA pamoja na CAF.

Mchezo kati ya Tp Mazembe dhidi ya Esperance hautakuwa na kiingilio na hivyo kila mtanzania na mpenda soka anaweza kwenda kesho Benjamin Mkapa kuwaunga mkono TP Mazembe.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments