Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi -
CCM Mkoa wa Singida MARTHA MLATA amewataka Viongozi wa Chama cha Mapinduzi na
Wananchi Mkoa wa Singida kuhakikisha wanaitunza Miradi iliyotekelezwa kupitia
Ilani ya CCM ili iweze kudumu kwa muda mrefu kutoa huduma kwa wananchi.
Mlata amesema hayo wilayani mkalama
wakati akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzu CCM Wilaya
ya Mkalama ambapo alisema kumekuwa na uharibifu kwenye baadhi ya miradi huku
viongozi na wananchi wakiwa wanaona.
Aliseama, hivyo ni wajibu wa kila mwana CCM na wananchi kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa na serikali katika maeneo yao inalindwa ili iweze kudumu kwa muda mrefu ikitoa huduma kwa wananchi.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Singida, walipata fursa ya kuzungumza na Wajumbe wa Mkutano ambapo walisema madiwani ni lazima wawasimamie watendaji kuhakikisha wanasoma mapato na matumizi kwenye mikutano ya hadhara ili kuwatoa hofu wananchi.
Walisema (Wajumbe) pia viongozi wa
CCM kuhakikisha wanasajili wanacha na kuendelea kuwakumbusha kulipa Ada kwa
wakati ili kuimarisha uhai wa Chama.
Jasmini Kinga ambaye pia ni mjumbe
wa kamati ya siasa mkaoa wa singida yeye alisisitiza kuwepo kwa mahusiano na
kuaminiana wakati wa kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo kwa uadilifu
katika jamii na taifa kwa ujumla.
Na Mwandishi Wetu Kutoka Singida
0 Comments