Kocha wa makombe atua Simba SC

SIMBA SC imemtangaza Abdelhak Benchikha raia wa Algeria kuwa kocha mkuu wa klabu hiyo akichukuwa nafasi ya Roberto Oliveira ‘Robertinho’.

Adelhak aliipa ubingwa klabu ya USM Alger wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Yanga SC msimu wa 2022-2023.

Miongoni mwa timu kubwa Afrika alizowahi kufundisha ni CR Belouzdad, MC Alger, USM Alger, ES Setif ya Algeria, Club Africain ya Tunisia, Raja Casablanca, Difaa El Jadida na RS Berkane vya Morocco.

Simba iliachana na Robertinho wiki tatu zilizopita baada ya makubaliano ya kuvunja mkataba kwa pande zote mbili.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments