Nape: Mifumo ya Hospitali kuunganishwa

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema kuwa hospitali zimekuwa na mifumo mingi na haisomani kiasi ambacho imechangia kuongezeka kwa gharama za matibabu kwa wananchi.

Waziri Nape ameyasema hayo wakati akifunga maonesho ya tatu ya kidijitali ya Afya na Ubunifu yaliyoandaliwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili katika kampasi ya Mloganzanziala, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Vyombo vya Habari mara baada ya kufunga mafunzo hayo Waziri Nape amesema maonesho hayo yamewakutanisha wadau mbalimbali ndani na nje ya Nchi ili kujadili namna TEHAMA inavyoweza kuboresha huduma za Afya.

“Tunataka kwa kupitia TEHAMA tuboreshe huduma hiyo ili mtu akienda kokote taarifa zake ziwepo,” amesema Waziri Nape.

Waziri Nape ameeleza jitihada mbalimbali zinazofanyika chini ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kufanya mifumo ya TEHAMA isomane ili kuweza kupunguza gharama kubwa ya matibabu kwa wananchi Pamoja na zile za uendeshaji.

Pa Waziri Nape amesema Kuna uwekezaji mkubwa umefanyika kwenye mkongo wa Taifa wa mawasiliano ambao ndo njia kuu ya kupeleka hizo taarifa na kuna mifumo kadhaa lazima itengenezwe ili taarifa ziwe pekee kwa kila mtu.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments