WAZIRI MSTAAFU MHE. PINDA ATEMBELEA MAONESHO YA WIKI YA HUDUMA ZA FEDHA

Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda (kulia), akisikiliza kwa makini maelezo kuhusu namna ya utekelezaji wa miradi kwa njia ya ubia, kutoka kwa Kamishna Msaidizi, Idara ya Ubia kati ya Sekta Binafsi na Sekta ya Umma (PPP), Bw. Bashiru Taratibu, alipotembelea banda la Wizara ya Fedha, wakati wa Maadhimisho ya Tatu ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Uchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha. Maadhimisho hayo yanawakutanisha Taasisi ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka mkoa wa Arusha.


Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda (wa pili kulia), akizungumza na Maafisa wa Idara ya Sera kutoka Wizara ya Fedha, Bw. Abdul Ndachi (wa pili kushoto) na Bi. Mwanaidi Kanyawanah (kushoto), katika Maadhimisho ya Tatu ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Uchumi” , yanayoendelea katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha. Wa kwanza kulia ni Kamishna Msaidizi wa Idara ya Uendelezaji wa Sekta ya Fedha, Bi. Janeth Hiza. Maadhimisho hayo yanawakutanisha Taasisi ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka mkoa wa Arusha.


Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda (kushoto), akisikiliza maelezo kuhusu malipo ya pensheni na mafao ya uzeeni kwa wastaafu kutoka kwa Afisa Hesabu Mwandamizi kutoka Idara ya Mhasibu Mkuu wa Serikali, Bw. Fadhili Izumbe (katikati) alipotembelea Maadhimisho ya Tatu ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Uchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha. Maadhimisho hayo yanawakutanisha Taasisi ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka mkoa wa Arusha Kushoto ni Mhasibu Mkuu, Bi. Joyce Chaki.


Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Banda la Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ), katika Maadhimisho ya Tatu ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Uchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha. Maadhimisho hayo yanawakutanisha Taasisi ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka mkoa wa Arusha. Akishudiwa na Bi. Aziza Baraka Omar, Afisa Masoko wa Banki hiyo na Bw. Hassan Khamis Hamad, Afisa Mauzo wa Benki hiyo.


Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda akimsikiliza kwa makini Mwanasheria wa Serikali kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi, Bi. Antelma Mtemahanji, kuhusu taratibu za usajili wa vikundi alipotembelea Maadhimisho ya Tatu ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa, yenye kaulimbiu “Elimu ya Fedha, Msingi wa Maendeleo ya Uchumi”, yanayoendelea katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha. Maadhimisho hayo yanawakutanisha Taasisi ndogo za Fedha, Benki, Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na wajasiriamali kutoka mkoa wa Arusha.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Arusha)

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments