Wanawake Dodoma changamkieni fursa za kiuchumi

DODOMA: MBUNGE wa Jimbo la Dodoma Mjini  Anthony Mavunde amewataka wanawake wa Dodoma kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo mkoani hapo ili kujiinua zaidi.

 

Mavunde ameyasema hayo leo  akiongea na wakina mama wajasiriamali wa Dodoma ambao walikuwa wakisheherekea miaka mitatu tangu kuanzishwa kwa US AS ONE-KICOBA

“Ninawapongeza sana kwa muunganiko huu wenye dhamira ya kuinuana kichumi kupitia VICOBA.

 

“Kwa miaka mitatu tangu kuanzishwa kwenu mmepiga hatua na kupata mafanikio makubwa ikiwemo kuongeza mtaji mpaka kufikia milioni 63,” amesema Mavunde

Amesema, serikali chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu  Hassan imefanya kazi kubwa ya kuweka mazingira rahisi ya uwekezaji Jijini Dodoma na hivyo kuongeza wigo mpana wa kiuchumi.

 

“Hivyo nitoe rai kwenu kutumia fursa hii kubwa kushiriki katika shughuli za kiuchumi ili kujiongezea kipato na kukuza uchumi wenu,kama Mbunge wenu nitakuwa tayari kuwashika mkono na kuwaongoza vyema,” amesema

Akisoma risala, Mwenyekiti wa US AS ONE-KICOBA, Pauline Chuma  amesema madhumuni yao hivi sasa ni kukua kutoka KICOBA kwenda kuwa SACCOS ili kutanua wigo wa shughuli zao sambamba na kuongeza idadi kubwa ya wanachama ili kuunganisha nguvu kwa pamoja.

Akitoa shukrani kwa niaba, Katibu wa US AS ONE-KICOBA amemshukuru Mavunde kwa kukubali ombi lao la kuwa mlezi wao pamoja na kuwachangia sh milioni3 za ununuzi wa vifaa vya kupikia.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments