Bima ya afya haiepukiki – Rais Samia

RAIS Samia Suluhu Hassan amesema ili kuendelea kutoa huduma za afya endelevu suala la bima ya afya kwa kila mtu haliepukiki.

Rais Samia ameyasema hayo leo Januari 10, 2024 katika ufunguzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mjini Magharibi (Lumumba)

Mfuko wa bima ya afya

Amesema, hospitali hiyo ya Lumumba itasaidia kupunguza msongamano wa wagonjwa na kutoa huduma bora zinazokusudiwa.

“Suala la bima ya afya haliepukiki tujipange kila mmoja kuwa na bima ili tutibiwe vile ipasavyo,” amesema.

Pia ameeleza kufarijika kuwepo kwa wataalamu katika hospitali hiyo, na kutoa rai kwa Wizara ya Afya kuhakikisha inaendelea kutoa huduma bora kwa wananchi.

VIDEO: MSIACHE KUTUMIA OFISI ZETU KWA MSAADA WA KISHERIA

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments