DC amsimamisha kazi afisa elimu

  

 Mkuu wa Wilaya ya Tanga, James Kaji amemuagiza Mkurugenzi wa  jiji la Tanga, Said Majaliwa kumsimamisha kazi afisa elimu shule za sekondari  Lusajo Gwakisa  kwa tuhuma za  kukiuka muongozo wa serikali  katika kusaini mkataba wa  ujenzi wa madarasa na majengo ya utawala kwenye   shule mpya  ya sekondari kiomoni .

Agizo hilo amelitoa  mara baada ya kukagua ujenzi wa shule mpya ya sekondari ya kata ya Kiomoni ambayo inatekelezwa kupitia mradi wa SEQUIP ambayo mpaka sasa ujenzi wake haujakamilika.

Ameelekeza kuwa mradi huo unatakiwa ukamilike ifikapo Januari 15 ili wanafunzi waweze kuanza masomo yao katika shule hiyo mpya bila ya changamoto zozote zile

“Nakuagiza mkurungenzi wa jiji msimamishe afisa elimu lakini ajieleze na uchunguzi ufanyike juu ya sababu ya kusaini  mikataba ya ujenzi kinyume na taratibu za serikali zilivyoelekeza”amesema DC Kaji.

Hata hivyo Mkurungenzi wa jiji, Saidi Majaliwa amesema kuwa mradi huo upo zaidi ya asilimia 50 ya utekelezaji wake na unatarajiwa kukamilika Januari 15 mwaka huu.

“Hapa sio kwamba kuna uhaba wa madarasa hapana tulikuwa tunaongezea majengo ya utawala na maabara ili watoto waweze kuhamia hapa kutoka shule ya awali na kuendelea na masomo yao katika mazingira mazuri “amesema mkurungenzi huyo.

Amesema kutokana na shule ya awali kuwa na changamoto ya kiafya kutokana na kuwa karibu na eneo la viwanda vya kuzalisha chokaa hivyo waliamua kuhamishia shule katika eneo hilo jipya.

Hata hivyo alisema kuwa kutokana na changamoto hizo gharama za ujenzi wa shule hiyo ziliweza kuongeza kutoka Sh milioni 584 zalizotengwa hadi kufikia zaidi ya Sh milioni 700.

Wananchi wa kata ya Kiomoni wameiomba serikali kuharakisha ujenzi wa shule hiyo ili wanafunzi wasiendele kupata changamoto za kiafya katika shule ya awali.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments