John Okello alikuwa akiishi Pemba ambako
alitokea Uganda miaka michache na akiwa ndani ya Zanzibar alipata umaarufu kwa
vijana mahiri, ambao wengi wao walikuwa wabeba mizigo na wachukuzi wa meli
zilizoingia na kutoka Bandarini Zanzibar.
Kundi la John Okello lilikutana kwa siri.
Okello aliwapa matumaini ya mabadiliko wafuasi wake, ambao walikuwa wakifanya
kazi pamoja kwa muda mrefu na mara nyingine katika mazingira ya hatari, wakiwa
na utayari wa kufuata amri za kiongozi yeyote ambaye ataweza kuwalipa, kiufupi
walikuwa waasi wanaotafuta makazi.
Mchafuko wa kisiasa ulikuwa ukiongezeka
ndani ya Zanzibar na Pemba tangu kifo cha Sultani Khalifa mwaka 1960. Sultani
Khalifa alitawala Zanzibar miaka ya 50, tangu mwaka 1911.
Baada ya udanganyifu mkubwa kwa majimbo ya
uchaguzi na mseto katika chaguzi kuu mbili za mwaka 1961, vyama vikuu
vilishindwa kujipatia wingi wa kura kwa kila kimoja.
Waingereza waliondosha majeshi yao kikiwemo
kikosi maalumu cha Kiarishi ambacho kilikuwa kimewekwa karibu na uwanja wa gofu
na mpaka wa mji mkongwe mapema mwaka 1963.
Wakati mfalme mpya, Jemshid akipandisha
bendera ya Taifa huru la Zanzibar tarehe 12 Desemba 1963, aliadhimisha
uondokaji wa Gavana wa kiingereza Zanzibar na mwisho wa ukoloni Zanzibar.
Uchaguzi mwingine uliofanyika mwishoni mwa
mwaka 1963 ukiipa ushindi mdogo wa kura Muungano wa vyama viwili ZNP na (chama
cha kizalendo Zanzibar) na ZPPP (Chama cha watu wa Pemba na Unguja).
A.S.P (Chama cha Afro shirazi) kilikuwa
kiwe kipo katika Serikali iliyo na chini ya nusu ya wabunge kwa mtindo wa bunge
la Kiingereza na Sultani, akiwa kama ni mtawala tu lakini sio mtawala mwenye
maamuzi ya mwisho.
Taifa hilo la Zanzibar, ambalo lilikuwa
mwanachana kamili wa Jumuia ya madola na mwanachana mpya wa Umoja wa Mataifa
lilidumu kwa siku 33 pekee, ambapo majadiliano mazito ya kisiasa na maandamano
yalikuwa ni matukio ya kawaida wakati huo.
Makundi ya watu yalikuwa yakiimba na kusifu
majina mbalimbali ya viongozi wa kisiasa, huku yakivuka vizuizi vya barabara
vilivyokuwa vikilindwa na askari wa kiingereza.
Vikundi vilijadiliana juu ya mambo
mbalimbali, mfano haki dhini ya fursa, Wageni dhidi ya wenyeji wa zamani,
Ubepari dhidi ya Ujamaa, Wafanyabiashara dhidi ya wamiliki ardhi, Waunguja
dhidi ya Wapemba, Waasia dhidi ya pazia la nyuma la vita baridi na harakati za
utaifa na kuondosha ukoloni ambao ulikuwepo kipindi hiki ndani ya Afrika.
John Okello hakuwa na jawabu ya mambo haya
nyeti, lakini alikuwa na kipawa cha kutambua kwamba vikundi hivi
vinavyoshindana, vinatoa nafasi nzuri kwa mtu wa harakati kama yeye.
Hata hivyo, watu kama 100 waliojidhatiti
wangaliweza kutwaa vituo muhimu vya kienyeji vya habari na kambi za Polisi mara
baada ya vituo vya habari na Kambi za Polisi pamoja na silaha kudhibitiwa na
John Okelo.
Ni nani katika visiwa angeweza kumshinda?
Je, wanasiasa wangeliungana na kumshutumu na kumpinga kwa vitendo vyake visivyo
halali? Au kama alivyotaraji, wangeendelea kutoaminiana na kutuhumu kwamba kati
yao ndio wanaomuunga mkono? Jee, wasingelitaka kukubaliana na yeye, haraka
kabla mwengineo hajafanya hivyo? John Okello aliwachezesha usiku huo wa
Januari.
Viongozi wa A.S.P walifadhaishwa na matendo
ya Okello (wengi wao, walikuwa hata hawapo visiwani wakati huo) hivyo
wakakimbilia haraka kuwaunga mkono waasi.
Mamia ya wafuasi wa vyama walipigwa na
butwaa juu ya wale ambao walikuwa na shuku ya kukata fundo hilo gumu la
majadaliano ya kidemokrasia na kukimbilia moja kwa moja kwenye utawala.
Hawa walitafuta njia ya kuiandaa jamii
kwenda sambamba na kanuni zao. Kanuni siku hizo zilikuwa ni ghali sana kama
sarafu ya Marekani. Ubinadamu ulikuwa ni kitu adimu sana.
Baadhi ya viongozi wa ASP baada kuona
kwamba Serikali itakuwa haina udhibiti na uwezo kujilinda na kutokuwa na imani
matokeo ya chaguzi huria zilizofanyika, walitafuta njia za haraka za
kuhalalisha udhibiti wa yale ambayo yaliitwa sasa “Mapinduzi”.
Makundi ya watu wenye fujo yalikuwa huru.
Sheria na amani zilikuwa hazipo katika mitaa ya Zanzibar na walimiliki ardhi na
wafanya biashara waliburutwa kutoka majumbani na madukani mwao, uporaji na
mauaji yalienea mji mkongwe mzima. Kwa kweli mji wenyewe uliporwa.
Waarabu na Waasia , waliokuwa wakiunga
mkono vyama vyengine waliuliwa kwa makundi. Kwa usiku mmoja maisha ya watu
yasiyovika yalipotea na siku nyengine baadae maelfu ya watu waliikimbia nchi
pamoja na kila walichoweza kubeba.
John Okello mwenyewe alijipachika cheo cha
Jemedari Mkuu akishirikiana na bataliani zake zenye fujo walianzisha utawala wa
vitisho ndani ya visiwa vya Unguja na Pemba.
Okello alitangaza vitisho visivyo vya
kawaida na ahadi ya kifo kwa wote watakaojaribu kumpinga akuamini alikuwa
akipokea maelekezo /dokezo kutoka kwa Mungu na akionyesha uwezo usiokuwa wa
kawaida kwa kutumia nambari, kwa mfano Januari 13, 1964, alitangaza ujumbe.
Alisema, “Serikali sasa inaendeshwa na sisi
ikiwa mtakuwa wakaidi na kukataa kutii amri, Nitachukua hatua kali mara 88
zaidi ya hatua ninazozichukua hivi sasa, ikiwa yeyote atashidnwa kutii amri ya
kutotoka nje ya nyumba kama walivyofanya wengine.sitokuwa na njia nyengine
lakini kutumia silaha nzito. Sisi, ni jeshi lenye nguvu ya 99,099,000.”
Vitisho vyake na uwezo wake wa kuvitekeleza
viliwatia hofu raia, hasa makundi mbalimbali ya jamii zilizo ndogo. Na baadaye
Januari 14, 1964 alitangaza maneno ya kufadhaisha akisema, “huyu hapa ni
Jemedari Mkuu wa Unguja na Pemba, nafikiria kuelekea kijiji cha Mtendeni
kukiangamiza ikiwa watu wa hapo hawatafuata amri.”
“Baada ya dakika 40 nitawamaliza nyote hasa
Wangazija na kwa vijana wote wa kiarabu wanaoishi Malindi. Nitapita Malindi
nikiwa nimesheheni silaha ambazo mimi mwenyewe ndie nizijuazo. Nataka kuona
kila mmoja amelala chini. Nataka kuwaona wao wanaimba… Baba wa Waafrika. Mungu
Mbariki yeye na malengo yake na yale ya Jemedari Mkuu,” alisisitiza Okello
Wakati unyanyasaji uliposima jamii za
tamaduni tofauti za Zanzibar zilikuwa zimeparaganyika. Taifa la chama kimoja
lilitangazwa. Lakini bado Taifa hili likihofia uwezekano wa kufufuka upinzani
kutoka kwa wapinzani waliokimbia nchi.
Wanamapinduzi hawa baadae walijihakikishia
udhibiti zaidi baada ya kusaini mkataba wa muungano wa Tanganyika. Hii
ingeruhusu maelfu ya marafiki wa kisiasa wa Tanganyika kuingilia kati upinzani
wowote wa baadae katika visiwa hivi.
Askari Polisi wa Zanzibar walibadilishwa
kwa askari Polisi kutoka Tanganyika ambao ni watiifu kwa chama na pazia la
siasa za utengano ziliwakumba wazanzibari ambazo zilitakiwa kudumu kwa zaidi ya
miaka 20.
Leo hii siasa hizi za utengano hazipo tena,
kumalizika kwa vita vya baridi na kuelekea kwa uchumi wa kisasa umeweza
kuifungulia Zanzibar milango kwa ulimwengu wa nje.
Uchaguzi wa vyama vingi ulifanyika mwaka
1995 halafu tena ukafanyika mwaka, 2000 na baadaye 2005 na kuendelea. Viongozi
wa kweli na wenye kujali hali za watu wameonekana.
Hii imewafanya wakimbizi waliokimbia wakati wa mapinduzi kurejea visiwani. Uvumilivu na amani wa watu wa aina tofauti, ambayo ni tabia ya maisha ya wazanzibari, ulirejea katika mitaa ya mji mkongwe na amaki ikapatikana hadi hii leo ambapo tunashuhudia Demokrasia ikizudi kuchanua.
0 Comments