MWENEZI MAKONDA AWASIHI WATAALAM WA SERIKALI KUTUMIA TAALUMA ZAO KATIKA KUWASADIA WAZEE

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndugu. Paul Makonda amewataka Wataalam wa Halmashauri, Taaisi na Idara mbalimbali Serikalini kutambua kwamba neema ya maisha yao imetokana na Wananchi waliopiga kura kwa kukicchagua Chama Cha Mapinduzi na kuunda Serikali.

Akizungumza na Wananchi waliojitokeza kwa wingi katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Manyara kwa kuwasilisha kero na Changamoto zao ikiwa ni agizo la CCM kwa RC Manyara.

ISOME NA HII >>PICHA: SENDIGA ATEKELEZA AGIZO LA MAKONDA

Mwenezi Makonda amewasihi Wataalam kutoa huduma kwa upendo kwa kutoa muda wa wananchi kujieleza.

"Niwasihi wataalam toeni  huduma kwa upendo kwa wananchi hawa kwa kuwapa muda wa kujieleza na msikae kwa kuamini zaidi makaratasi kwani wakati mwengine watu hutumia nyaraka za kugushi kumdhulumu mwananchi asiye na uwezo, lazima tuelewe hilo na tutumie utaalamu wetu kuwasaidia zaidi wazee) Alisema Mwenezi Makonda.

Makonda ametoa rai kwa Wananchi kuwaamini Chama Cha Mapinduzi kwani pamoja na yeye kuondoka Manyara kuelekea Singida lakini bado chama kinaacha watu wake kufuatilia mwenendo mzima wa zoezi hilo na kubainisha kuwa aliwasiliana na Waziri wa TAMISEMI Ndugu. Mohammed Mchengerwa ambaye alimthibitishi watapokea taarifa zote za chama juu ya Watendaji na Watumishi wa Serikali ambao hawatafanya wajibu wao.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments