NAIBU WAZIRI WA MAJI MARYPRISCA MAHUNDI ATEMBELEA MIRADI YA MAJI LUSHOTO

 

Naibu Waziri wa Maji  Mhe. Maryprisca Mahundi amefanya ziara wilayani Lushoto kukagua utekelezaji wa miradi ya Maji ukiwemo mradi wa Kijiji cha Kibohelo kata ya Magamba Wilayani Lushoto mkoani Tanga.

Akiwa katika mradi huo Naibu Waziri Mahundi amewataka Wakandarasi kuhakikisha wanashiriki kutekeleza miradi hiyo hiyo na kumaliza kwa wakati ili kutoa huduma hiyo kwa wananchi.

Aidha Naibu waziri Maryprisca amemuagiza Meneja wa Wakala wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA Wilaya Lushoto Erwen Sinzinga kuwachukulia hatua watumishi wawili wanaofanya uzembe katika mradi wa Nyankhei uliopo kata ya Ngulwi wilayani Lushoto

Chanzo Malunde blog

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments