RAIS SAMIA ATUMA SALAMU ZA POLISI VIFO VYA WATU ZAIDI YA 21 MGODINI SIMIYU

Picha mfano wa shimo mgodini

 Wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu zaidi ya 21 wamefariki dunia kufuatia ajali ya kufunikwa na ardhi katika Mgodi wa Ng'alita, Wilaya ya Bariadi, mkoani Simiyu.

Inaelezwa kuwa tukio hilo limetokea baada ya kudaiwa kuingia mgodini kwa kujipenyeza kinyume cha sheria kwani shughuli za uchimbaji zilikuwa zimesitishwa.

Kufuatia ajali hiyo iliyotokea saa 11 alfajiri Januari 13,2024 , Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametuma salamu za pole kwa ndugu, jamaa na marafiki waliopoteza jamaa zao katika ajali hiyo na kwamba Vyombo vya ulinzi na usalama vikishirikiana na uongozi wa mkoa vinaendelea na juhudi za kutafuta miili mingine ambayo bado imekwama ndani ya kifusi.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments