TFF: Kauli Za Amrouche Hatuzitambui

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia amesema shirikisho hilo haliungi mkono kauli ya kocha Adel Amrouche kwamba Morocco inapanga muda na waamuzi wa michezo yao.

“Sisi kauli yetu tunayoitoa tuko mbali na kauli zake na hatuzikubali, na tunajua tutafanya nini tuko kwenye mashindano, kuchukua hatua ambazo tutaona tunastahili kuchukua.” amesema Karia.

Mapema leo akiwa nchini Ivory Coast wakati akizungumza na waandishi wa habari, kocha huyo alisema Morocco inapanga ratiba za mechi zao na waamuzi pia.

Karia amesema shirikisho litaongea na kocha huyo kudhibiti kauli zake ili kuepuka changamoto zingine zinazoweka kuwakuta.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments