Makonda alitoa agizo
hilo Mkoani Singida, katika kijiji cha Sagara Wilaya ya Singida, wakati
akitokea mkoani Manyara akiwa katika Ziara yake ya kuimarisha Chama na kusikiliza
na kutatua kero za wananchi.
Alisema Serikali
imetoa fedha nyingi na Vifaa kwa ajili ya Maafisa Kilimo ili waweze
kuwatembelea wakulima kuwapa ushauri juu ya kilimo bora, lakini baadhi ya
Wakurugenzi wamekuwa changamoto kwa kuwatumia Maafisa Kilimo hao kama wakusanya
ushuru.
#HABARI: Tangu umeingia wewe katika nafasi ya Uenezi ya CCM Taifa hakika umeweka hamasa kubwa katika chama chetu, umeamsha mizi ambayo ilikuwa imelala Soma Zaidi - https://t.co/UhdtxyFx6r pic.twitter.com/tyiUyfnzdH
— Bandola Media (@bandolamediatz) January 25, 2024
Aidha alisema Chama hakitawavumilia wakurugenzi na viongozi ambao wanakwamisha juhudi za Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan za kuinua Sekta ya Kilimo.
Hata hivyo pia alimuagiza Waziri wa Kilimo Hussen Bashe kuhakikisha anawachukia hutua maafisa Kilimo ambao wanashindwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu.Alisema akishindwa
kuwachukulia hatua, Chama kitachukua hatua juu yake na kwa watendaji hao.
Baadhi ya wananchi wa
kijiji cha Sagara Wilaya ya Singida waliasema wanakabiliwa na changamoto ya
ubovu wa baadhi ya Barabara ambazo ni muhimu kwa shughuli mbalimbali za
kijamii.
#HABARI: Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndugu. Paul Makonda amewataka Wataalam wa Halmashauri, Taaisi na Idara mbalimbali Serikalini kutambua kwamba neema ya maisha yao imetokana na Wananchi - https://t.co/wDo3dkHksL pic.twitter.com/VU26YwqA0z
— Bandola Media (@bandolamediatz) January 25, 2024
Walisema ubovu wa
Barabara hizo imekuwa ni changamoto kubwa kwa akina Mama hasa wakati wa kufuata
huduma mbalimbali ikiwemo huduma za Afya.
0 Comments