BALOZI KIBESSE ATETA NA GAVANA WA KISUMU, PROF.ANYANG NYONG'O

Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dr. Bernard Kibesse amefanya ziara katika Kaunti ya Kisumu ambapo amekutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Prof. Peter Nyon’go, Gavana wa Kaunti ya Kisumu tarehe 8 Februari 2024.

Mhe. Balozi Kibese na Gavana Nyong’o wamekubaliana kuandaa mkutano wa ujirani mwema kati ya mikoa ya Tanzania na Kenya inayopakana kwenye eneo la Ziwa Victoria ili kuweka mikakati ya kuimarisha ushirikiano wa kijamii, kibishara na kiusalama katika maeneo hayo ikiwemo Mwanza na Mara kwa upande wa Tanzania na Kisumu na Migori kwa upande wa Kenya

Vilevile wamekubaliana kufuatilia mpango wa kuwa na miundombinu ya pamoja hususan barabara inayopita kwenye mwambao wa Ziwa Victoria upande wa Tanzania na Kenya.

Gavana Nyong'o amemzawadia Balozi Kibesse kitabu ambacho ameandika.





TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments