Wahitimu 40 wa vyuo mbalimbali nchini ambao wanatarajia kuanza mpango wa mafunzo kazini kwa vitendo unaodhaminiwa na kampuni ya GGML kwa mwaka 2024/2025 wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kukaribishwa rasmi mwishoni mwa wiki mkoani Geita.
NA MWANDISHI WETU
KATIKA kudhihirisha dhamira ya kuwajengea wahitimu wa vyuo mbalimbali kukubalika kwenye soko la ajira, Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imezindua mafunzo tarajali kwa wanafunzi 40 waliohitimu vyuo mbalimbali nchini.
Mafunzo hayo yanayotolewa kwa muda wa mwaka mmoja (2024/2025), yatahusisha programu mbalimbali ikiwamo za uanagenzi, mafundi mchundo, watalaam wa masuala ya madini ya fani nyingine ambazo zimeanzishwa ili kukuza ujuzi wa vijana wa kitanzania.
0 Comments