Dk. Mwinyi Amshukuru Samia Msiba wa Mwinyi

 Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwa bega kwa bega tangu Rais wa awamu ya pili, hayati Ali Hassan Mwinyi alipoanza kuugua mwezi Novemba na kupelekwa Uingereza kwa matibabu.

Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo leo Machi 3, 2024 katika hitma na dua maalum ya kumuombea kiongozi huyo ilyoandaliwa na Rais Samia katika viwanja vya maonesho Nyamanzi, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja.

Aidha, Rais Mwinyi amewashukuru pia Madaktari wa Hospitali ya Mzena kwa kazi kubwa waliyoifanya kujaribu kuokoa maisha ya Mzee Mwinyi pamoja na masheikh, waalimu, ndugu, marafiki na wananchi kwa dua nyingi walizomuombea Mwinyi kwa kupindi chote alichokuwa akiugua na baada ya kufariki.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments