GAVU AFUNGA MAFUNZO YA VIONGOZI WANAWAKE MIKOA 9 JIJINI MWANZA

Katibu wa NEC Idara ya Organaizesheni na Mlezi wa Jumuiya zote za Chama Cha Mapinduzi Ndg. Issa Gavu amefunga Mafunzo Maalum kwa Viongozi wanawake Kutoka mikoa 9 ya Kanda ya ziwa na kanda ya ziwa Magharibi.


Comred Issa Gavu amefunga mafunzo hayo yaliyohudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Chama na Jumuiya ya wanawake Tanzania wakiongozwa na Mwenyekiti wa UWT Ndg. Mary Chatanda yaliyofanyika Mkoani Mwanza .

Lengo la Mafunzo haya ni kuwajengea uwezo wanawake namna ya kuchochea Maendeleo ya Nchi na kuleta ufanisi wa Utendaji kazi katika Jamii na kujikwamua Kiuchumi.

Comred Issa Gavu amewasihi Viongozi wanawake waendelee kuunga Mkono Juhudi za Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, yeye ndiyo Mfano mzuri wa wanawake wote wanao onyesha kwa vitendo kujikwamua kiuchumi na ufanisi mzuri wa kazi, na yeye ndiye anawawakilisha katika ngazi ya Juu ya Uongozi wa Nchi.

Mafunzo hayo yaliyofungwa Mkoani mwanza katika Ukumbi wa Winterfell yamehusisha viongozi kutoka Mikoa ya Mwanza, Kagera, Katavi,Shinyanga, Simiyu,Geita, Kogoma,Tabora na Mkoa wa Mara leo Tarehe 27 Machi 2024.







TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments