Wawili wapoteza maisha ajali Kenya

WATU wawili wanahofiwa kufa baada ya gari la shule ya wavulana Kapsabet kupinduka katika Jimbo la Baringo nchini Kenya leo.

Taarifa ya mtandao wa NTV Kenya, iliyotolewa muda huu imeeleza kuwa waliokufa ni mwalimu na mwanafunzi.

Kwa mujibu wa mtandao wa Nation, polisi imetaja chanzo cha ajali ni dereva kupoteza mwelekeo alipojaribu kukata kona na gari hilo kuangukia kwenye bonde.

Kamanda wa polisi eneo hilo, Stephen Kutwa amesema basi hilo lilibeba wanafunzi 61 na mwalimu mmoja. Hata hivyo majeruhi wamewahishwa hospitali.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments