WANANCHI WATAKIWA KUENDELEA KUMUUNGA MKONO RAIS DK. SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

Waziri wa Fedha, ambae ni Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Dk. Mwigulu Nchemba ameendelea kuwaomba wananchi kuendelea kumuunga mkono Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa sababu ameendelea kuwajali wananchi wake kila eneo kuna miradi inayogusa wananchi.

Waziri wa Fedha Dk. Mwigulu alizungumza akiwa katika ziara Jimboni kwake   wakati akiongea na wananchi wa kata ya Old Kiomboi wilayani Iramba mkoani Singida.

Ameeleza  Rais Dk. Samia ameendelea  kujenga miundombinu ya barabara na shule mpya za msingi na sekondari nchini.

Akizungumzia kuhusu elimu, Dk. Mwigulu amesema katika uongozi wa Rais huyo,  amefanya makubwa katika wilaya hiyo ikiwemo kuwezesha shule mbili za kidato cha tano na sita ambapo mwaka huu zitaanza kupokea wanafunzi.

Aidha, amebainisha  kuwa  shule hizo ni Shelui na Ndago sekondari  huku akiahidi kukamilisha shule ya ufundi.

NA Mwandishi Wetu Iramba Singida

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments