Ihefu Yanga, Coastal zatinga Nusu Fainali

TIMU za Ihefu ,Yanga, na Coastal Union  zimetinga Nusu Fainali ya Michuano ya Kombe la Shirikisho la CRDB baada ya  kushinda michezo yao ya Robo fainali.

Ihefu imefuzu hatua hiyo baada ya kuitoa Mashujaa ya Kigoma kwa penalti 4-3 baada ya timu hizo kutoka 0-0 katika dakika 90 mchezo uliofanyika Uwanja wa Liti, Singida, huku Coastal ikifuzu baada ya kuifunga Geita Gold bao 1-0 Uwanja wa Mkwakwani Tanga.

Yanga yenyewe imefuzu Nusu Fainali baada ya  kuifunga Tabora United mabao 3-0 Uwanja wa Azam Chamazi, ambapo timu ya nne itajulikana Ijumaa Mei 3, wakati Azam itakapocheza na Namungo katika uwanja huohuo.

Mabao ya Yanga yamefungwa na Azi Ki dakika ya 35, Kennedy Musonda dakika ya 66 na Joseph Guede dakika ya 83.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments