Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Singida Cheif Thomas Mgonto ametekeleza ahadi yake ya kuwapatia vifaa vya michezo shule ya Sekondari Unyahati iliyopo Wilaya ya Ikungi mkoaniSingida.
Hayo yamefanyika jana Shule ya Sekondari Unyahati wilaya ya Ikungi Mkoani Singida ambapo Mgonto amesema ya kuwa aliombwa kusaidia vifaa vya michezo katika shule kwa ajili ya kusadia wanafunzi na yeye ameweza kuitikia wito huo.
" Walimu na Wanafunzi wa shule ya Unyahati wameendelea kushukuru serikali na chama cha mapinduzi CCM Kwa Chief Thomas Mgonto ambae ni mjumbw wa kamati ya CCM Mkoa Wa Singida Kwa Kuendelea kuwajali na kuleta huduma mbali mbali shuleni hapo kwa maslahi mapana ya jamii na taifa kwa ujumla. Chief Thomas Mgonto amewapa jezi za mpira wa miguu za Wanaume na wanawake ametoa jezi za Mpira wa wavu mipira pamoja na Koni kwa ajili ya kufanyia mazoezi shuleni hapo
TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI
Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516
0 Comments