GHOROFA LAPOROMOKA KARIAKOO, RAIS ATOA MAAGIZO

 

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mpaka Sasa limefanikiwa kuwaokoa watu nane ambao walikwama kwenye jengo lililoanguka Kariakoo na tayari wamepelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Zoezi la uokoaji linaendelea kwa kuwakwamua watu ambao wamekwama katika ghorofa ya chini.
Kupitia mitandao ya kijamii Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameandika ujumbe ufuatao:

"Nimesikitika kupokea taarifa ya ajali ya kuporomoka kwa jengo la ghorofa katika Kata ya Kariakoo, Wilaya ya Ilala, Mkoa wa Dar es Salaam. 

Nimeuagiza Uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam, Jeshi la Polisi, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, na Idara ya Menejimenti ya Maafa kufanya kila linalowezekana kufanikisha zoezi la uokoaji na tiba kwa majeruhi. 

Wakati hilo likiendelea na tukimuomba Mwenyezi Mungu awape pona ya haraka majeruhi, tuwaombee pia utulivu na subra ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wenzetu wanaotafuta riziki zao katika eneo hili muhimu kibiashara nchini ambao kwa namna mbalimbali wameathiriwa na ajali hii."

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments