NAKOMOLWA alisema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Maluga wilayani Iramba akiwa katika ziara yake ya kuelekea sherehe za maadhimisho ya kuanzishwa kwa Chama cha Mapinduzi CCM Tarehe 5/2/1977.
Alisema Chama hakiwezi kubadili Rais kwani Rais Dkt SAMIA SULUHU HASSAN anatosha na anafaa kuendelea kuliongoza taifa kwa kipindi kingine cha miaka mitano ili aweze kuwaletea wananchi maendeleo.
Akiwa katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Kata hiyo ya Maluga wilayani Iramba, Wananchi waliomba serikali kuiboresha Zaharani ya Kata hiyo ambayo inakabiliwa na changamoto mbalimbali hali inayosababisha kufuta huduma Singida mjini, ambapo ni mbali.
Wananchi hao walisema Zahanati hiyo inakabiliwa na upungufu wa wahudumu wa afya na Vifaa Tiba, hivyo waiomba Serikali kuwaongezea wahudumu hao ili waweze kupata huduma za afya zilizobora na waache kwenda mbali kufuata huduma.
Lakini pia waomba kujengewa Wodi ya wazazi ili akina Mama wajawazito wasipate changamoto wakati wa kujifungua.
Akitolea majibu kuhusu Zahanati hiyo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wazazi CCM Mkoa wa Singida BERTHA NAKOMOLWA alisema changamoto hiyo ameichukua na ataiwasilisha kwa viongozi ili iweze kutatuliwa na wananchi waanze kupata huduma za afya katika Zahanati hiyo.
NAKOMOLWA alisema atashirikiana na Mbunge wa jimbo hilo na uongozi wa Mkoa ili juhudi za kuanza ujenzi zianze na kupeleka Vifaa Tiba kwa lengo la kutatua changamoto zilizopo hapo.
0 Comments