Vifaa hivyo vimekabidhiwa kwa timu mbalimbali za mpira wa miguu za kata hiyo ili kuhamasisha ushiriki wa vijana katika michezo, huku kombati zikikabidhiwa kwa vikundi maalum vitakavyohusika na kulinda usalama wa kura na mazingira katika kipindi cha uchaguzi kijacho.
Mhe. Kinyeto amesema kuwa hatua hiyo inalenga kuwajengea vijana moyo wa uzalendo, ushirikiano, na kuwapa nafasi ya kushiriki katika maendeleo ya kijamii na kisiasa.
Aidha, Diwani huyo ametangaza kuwa mashindano ya Kindai Cup yataanza hivi karibuni, yakihusisha timu kutoka mitaa yote ya kata hiyo. Mashindano hayo yanatarajiwa kuwa chachu ya mshikamano na uhamasishaji wa amani kipindi cha uchaguzi.
Wakazi wa Kata ya Kindai wamepokea hatua hiyo kwa furaha, wakieleza kuwa ni uthibitisho wa uongozi unaowajali watu na kuwekeza kwa vitendo katika maendeleo ya jamii.
Na Abdul Ramadhani Singida
0 Comments