Gwau & Matembe Watesa Tena Singida! Ushindi Mnono Kura za Maoni CCM

Mwanasiasa mahiri Martha Gwau na mchangamfu na Mnyenyekevu Aysharose Matembe wamethibitisha bado wana mvuto mkubwa wa kisiasa baada ya kushinda kwa kishindo katika mchakato wa kura za maoni za Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa nafasi za ubunge wa viti maalum mkoa wa Singida.

Kura hizo za maoni zilizofanyika Julai 30, 2025, zimewaweka wawili hao kileleni kwa kuibuka kidedea dhidi ya wagombea wenzao waliowania nafasi hizo ndani ya CCM. Ushindi huu umetafsiriwa kama ishara ya kuaminiwa kwao na wajumbe kutokana na mchango wao ndani ya chama na jamii kwa ujumla.

Wachambuzi wa siasa mkoani humo wanasema ushindi huu sio wa bahati, bali ni matokeo ya uaminifu, uadilifu na juhudi walizoweka katika kutetea maslahi ya wanawake na jamii ya Singida kwa ujumla.

Wanachama na wafuasi wa CCM wamefurika mitandaoni kuwapongeza viongozi hao huku wakieleza matumaini yao kuwa wataendelea kusimamia ipasavyo maendeleo ya wanawake na vijana mkoani humo.

"Hawa ni wanawake wa kazi! Ushindi wao umetokana na ukweli kwamba hawakuwahi kuwasaliti wananchi wala chama," alisema mmoja wa wanachama waliohojiwa.

Mchakato wa kura za maoni unaendelea kushika kasi mikoa mbalnaimbali nchini huku CCM ikijiandaa na uchaguzi mkuu ujao.

 Na ALIFU ABDUL Singida

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments