Mapokezi yao yaligeuka kuwa sherehe ya amani, mshikamano na matumaini, huku maelfu ya wananchi wakiimba nyimbo za hamasa na kubeba mabango ya kuonesha imani yao kwa viongozi hao wawili.
Mhe. Kingu na Mhe. Mgonto wameendelea kutambulika kama nguzo muhimu za maendeleo katika Ikungi, wakijipambanua kwa kutekeleza miradi mikubwa ya kijamii ikiwemo uboreshaji wa elimu, huduma za afya, miundombinu ya barabara, maji safi na kuendeleza vijana kupitia ajira na michezo.
Kwa sauti moja, wananchi wa Ikungi wameahidi kuendelea kuwaunga mkono viongozi wao waaminifu na wachapa kazi, wakisisitiza kuwa Kingu na Mgonto ndiyo tumaini la kupeleka Ikungi mbele zaidi katika maendeleo endelevu.
Abdul Ramadhani -Singida


0 Comments