DK NCHIMBI AWAHUTUBIA WANANCHI WA JIMBO LA KWELA,SUMBAWANGA VIJIJINI.

MGOMBEA mwenza wa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwahutubia Wananchi wa Jimbo la Kwela katika Uwanja wa Laela A,Sumbawanga Vijijini katika mkutano mdogo wa hadhara wa Kampeni leo Jumatatu Septemba 8,2025.

Baada ya kuwahutubia Wananchi,Dkt.Nchimbi alitumia nafasi hiyo pia kuwanadi wagombea Ubunge wa Mkoa wa Rukwa akiwemo Mbunge wa jimbo la Kwela,Deus Clement Sangu pamoja na Madiwani.

Dk.Nchimbi ameingia Mkoani Rukwa leo kuendelea na mikutano yake ya kampeni ya kutafuta kura za kishindo kwa Chama Cha Mapinduzi ( CCM) kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 29,2025.






TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments