Ametoa wito huo wakati wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi katika Jimbo la Iramba Magharibi, ambapo aliongoza mkutano wa hadhara iliyohudhuriwa na maelfu ya wananchi.
Katika hotuba yake, Bi. Mlata aliwaomba wananchi kuendelea kuwa imara katika mshikamanon na umoja, huku akihimiza mshikamano katika kulinda amani na maendeleo yaliyopatikana chini ya uongozi wa CCM.
![]() |
| “Tunapaswa kuendeleza amani tuliyo nayo kwa kuchagua viongozi wenye dira na maono ya taifa, viongozi wanaojali wananchi na masilahi ya taifa letu. Amani ndiyo msingi wa maendeleo,” alisema. |
Vilevile alimuombea kura Dkt. Mwigulu Nchemba, mgombea ubunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, na wagombea wote wa nafasi za udiwani katika kata mbalimbali za jimbo hilo.
Bi. Mlata alibainisha namna ambavyo Ilani ya CCM imetekelezwa kwa mafanikio makubwa katika kipindi kilichopita, na akawahakikishia wananchi kuwa utekelezaji zaidi utafanyika kwa kasi kubwa zaidi katika awamu inayofuata.
Amewakumbusha wananchi kuendelea kutunza vitambulisho vya kupiga kura na kuhamasishana kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura tarehe 29 Oktoba,2025 ili kuichagua CCM na viongozi wake wote kwa ushindi wa kishindo.
Matukio Mbali mbali kwa Picha katika uzinduzi huo.








%20-%20Copy.jpg)
%20-%20Copy.jpg)





0 Comments