Baada ya kufanya ziara za kusaka kura katika kata kwa kata, kijiji kwa kijiji na mtaa kwa mtaa mkoani Singida, Comrade Bertha Nakomolwa ameendelea kuwa sauti ya hamasa na mshikamano ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Akiwa ameonesha ari na uthubutu wa kipekee katika kampeni za chama, Nakomolwa amesema sasa ni wakati wa kukusanyika kwa pamoja wilayani Ikungi, ndani ya Jimbo la Ikungi Magharibi, kwa ajili ya kufunga kampeni kwa kishindo kikubwa kinachoashiria ushindi wa CCM katika uchaguzi unaotarajiwa.
Wananchi wengi wameendelea kumpongeza kwa uongozi wake wa mfano na jitihada za kuunganisha makundi mbalimbali ya vijana, wanawake na wazee katika kuhamasisha amani na mshikamano wakati wa kipindi hiki cha kampeni.
Na Abdul Bandola Singida
Wito wa Bertha Nakomolwa unalenga kuhakikisha kuwa CCM inaendelea kuandika historia ya ushindi, huku wananchi wakiahidi kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi kuhakikisha “Kura zote ni za kijani”.
Kwa kauli mbiu yake isemayo “Kura ya CCM ni kura ya maendeleo, amani na umoja wa kitaifa,” Nakomolwa amekuwa chachu ya uamsho mpya wa kisiasa ndani ya Mkoa wa Singida
Na Abdul Bandola Singida





0 Comments