Katika mkutano huo uliohudhuriwa na mamia ya wananchi, Hapi aliendelea kunadi Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kuwasihi wananchi kujitokeza kwa wingi tarehe 29 Oktoba 2025 kushiriki uchaguzi kwa kuwachagua wagombea wa CCM kuanzia ngazi ya Urais, Ubunge hadi Udiwani.
Kwa upande wake, Mwigulu Nchemba aliahidi kuendeleza kasi ya maendeleo kwa kuwaletea wananchi miradi mikubwa ya barabara, elimu, afya na kilimo, akisisitiza kuwa “Iramba ni ngome ya ushindi wa CCM, na maendeleo yataendelea kushamiri.”
Nakomolwa, ambaye ni kiongozi wa wazazi mkoani Singida, alihimiza mshikamano wa wanachama na wapenzi wa CCM, akiwataka wazazi na walezi kuhakikisha kura zote za “ndiyo” zinaelekezwa kwa wagombea wa chama hicho ili kulinda heshima ya ushindi wa kishindo mkoani Singida.
Baada ya mkutano huo, msafara wa Hapi uliendelea kuelekea mkoani Shinyanga kuendeleza hamasa na kampeni za chama.
0 Comments