MNEC wa Mkoa wa Singida Apongeza Mwenyekiti wa Wazazi Mkoa kwa Kuimarisha Jumuiya na Kuinadi CCM kwa Vitendo

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (MNEC) Mkoa wa Singida, ambaye pia ni mgombea ubunge wa Jimbo la Itigi, amempongeza Mwenyekiti wa Wazazi Mkoa wa Singida, Bi. Bertha Nakomolwa, kwa uongozi wake madhubuti na jitihada za kuifanya Jumuiya ya Wazazi kuwa imara, hai na yenye ushawishi mkubwa katika mkoa wa Singida.

Akizungumza wakati wa tukio la kisiasa lililohusisha viongozi wa chama, wanachama na wananchi, MNEC huyo alisema kuwa mwenyekiti huyo amekuwa mfano wa kuigwa katika kuendeleza taswira chanya ya CCM kupitia matukio yenye kuhamasisha umoja, upendo na maendeleo.

“Mama Nakomolwa amekuwa chachu ya uhai wa Jumuiya ya Wazazi. Anafanya kazi kwa vitendo, anaunganishi wananchi, na kila tukio analolisimamia linakuwa na tija kwa chama na jamii. Huu ndio uongozi tunaoutaka ndani ya CCM,” alisema MNEC huyo.

Aidha, amesisitiza kuwa hatua zinazochukuliwa na Jumuiya ya Wazazi mkoani Singida katika kuinadi Ilani ya CCM na kuwaombea kura wagombea wote wa chama hicho ni ishara ya uzalendo na uelewa wa hali ya kisiasa kuelekea uchaguzi wa mwaka 2025.
“Tukiwa na viongozi makini kama hawa, ushindi wa CCM si hadithi bali ni hakika. Tunawaomba wananchi waendelee kuiamini CCM kwa kuwa ndiyo chama kinachotekeleza ahadi zake kwa vitendo,” aliongeza.

Kwa upande wake, viongozi na wanachama waliohudhuria walipongeza ushirikiano wa viongozi hao wawili wakisema ni ishara ya umoja ndani ya chama na ni msingi wa ushindi mkubwa unaotarajiwa kwenye uchaguzi ujao.

Na Alifu Abdul Singida Itigi

 

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments