Historia itajirudia Kombe la Mapinduzi?

UNGUJA, Zanzibar: MLANDEGE FC wametinga fainali ya Kombe la Mapinduzi kwa mwaka wa pili mfululizo baada ya kuitoa APR kwa mikwaju ya penalti 4-2.

Dakika 90′ za mchezo zimemalizika kwa suluhu, ingawa dakika 3 kabla kutimia dakika 90, Masoud Rashid Juma wa Mlandege FC na Clément Niyigena wa APR wameoneshwa kadi nyekundu kwa mchezo usio wa kiungwana.

Macho na masikio yametega kutaka kungámua, nani kucheza fainali na Mabingwa watetezi wa Mapinduzi? Je, watafanikiwa kutetea taji?

Dakika 90’za mchezo wa kesho majira ya saa 2:15 usiku zitaamua, ima Singida Fountain Gate au Simba SC kumenyana na watetea ubingwa.

Simba na Singida wamepenya kutoka kundi moja. Mchezo wao wa siku 6 nyuma, Singida walikubali kichapo cha 0-2 dhidi ya mnyama.

Historia itajirudia?

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments