MKOA WA DODOMA WAPEWA HESHIMA NA DHAMANA YA KUANDAA SHUGHULI YA MAOMBOLEZO NA MAZISHI KITAIFA MACHI 22/2021

 


Na Jackline Kuwanda,Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samiah Suluh Hasan atongoza waombolezaji kuuga na kutoa heshima za mwisho kwa mwilii wa hayati Dkt John Pombe Magufuli Rais wa awamu ya tano katika uwanja wa Jamhuri Mkoani Dodoma.

Akizungumza leo na Waandishi wa Habari Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt Binilith Mahenge amesema Mkoa umepewa heshima na dhamana ya kuandaa shughuli ya maombolezo na mazishi kitaifa machi 22 mwaka huu.

‘’heshima hii tuliyopewa imezingatia nafasi aliyoipa mkoa wa Dodoma wakati wa uhai wake hasa kwa kubeba jukumu la kutekeleza azimio la siku nyingi la kuifanya Dodoma kuwa makao ya nchi na serikali’’Dkt Mahenge

Aidha amewahimiza wakazi Mkoani hapa kushiriki wingi katika shughuli ya maombolezo .

‘’Shughuli za kusaini kitabu cha maombolezo limeanza leo ,serikali imeandaa utaratibu mzuri wa viongozi ,wananchi na makundi mbalimali kushiriki kusaini kitabu hiki na itakuwa ni uwanja wa Nyerere Square’’Dkt Mahenge

Dkt Mahenge amesema, viongozi watakao shiriki ni pamoja na Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya  Zanzibar  Dkt Ally Husein Mwinyi ,viongozi wa kitaifa  ,viongozi wa Jumuiya,Taasisi za kimataifa ,Mabalozi na Viongozi kutoka nchi mbalimali.

Hatahivyo Dkt Mahenge amesema ulinzi na usalama umeimarishwa katika maeneo yote Mkoani hapa.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments