VIKAO VYA KAMATI ZA BUNGE KUANZA TAREHE 8 HADI 26 MACHI 2021

 Kamati za kudumu za Bunge zinatarajia kuanza kukutana siku ya Jumatatu wiki ijayo tarehe 8 hadi 26, Machi, 2021 ambapo Wabunge wote wanatakiwa kuwasili jijini Dodoma Jumapili  Tarehe 7 ,Machi, kwa ajili ya vikao hivyo.



Katika taarifa iliyotolewa kwa Vyombo vya Habari leo na kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa kimataifa, Ofisi ya Bunge imefafanua kuwa shughuli za kamati zitakakuwa katika kipindi hicho ni pamoja na   kupokea mapendekezo ya serikali kuhusu mpango, kiwango cha ukomo wa Bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kwa mujibu wa kanuni ya 116[1] ya kanuni za kudumu za Bunge toleo la Juni, 2020, wabunge wote watahusika.

Shughuli zingine  zitakazofanyika ni pamoja na kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi iliyotengewa fedha  kwa mwaka wa fedha 2020/2021  ili kuzingatia masharti  ya kanuni ya  117[1] ya kanuni za kudumu za Bunge  toleo la Juni 2020 ambapo wajumbe wa kamati za kisekta watahusika.

 

Taarifa  ya kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa kimataifa ,Ofisi ya Bunge iliendelea kubainisha kuwa shughuli zingine zitakazofanyika ni uchambuzi wa sheria ndogo zilizowasilishwa katika mkutano wa pili  wa Bunge ili kutekeleza  masharti ya kifungu cha 11 cha nyongeza ya Nane  ya kanuni za kudumu za bunge  toleo la Juni,2020 na mashauriano kati ya kamati ya Bajeti kuhusu masuala muhimu yatakayokuwa yamejitokeza kwenye kamati za kisekta  wakati wa uchambuzi wa taarifa  za utekelezaji wa Bajeti  kwa mwaka wa fedha 2019/2020.

TUANDIKIE MAONI YAKO HAPA CHINI

Je, wewe ni Mfanyabiashara na Unatamani Kutangaza Bidhaa Zako Kupitia Tovuti/Blog Yetu? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia bandolaonline@gmail.com au WhatsaApp: + 255 766 365 560 au 0652 388 516

Post a Comment

0 Comments